Wednesday, 30 November 2016

Usalama wa Ajira



Hati ya Maandishi ya Ajira
Sheria ya kazi ya Tanzania inahitaji kwamba wafanyakazi wapewe mkataba ulioandikwa wa ajira wanapoanza ajira isipokuwa kwa wale ambao wanafanya kazi chini ya siku 6 kwa mwezi kwa mwajiri fulani. Huenda mkataba wa ajira ukuwa wa kipindi chenye kikomo au kisichokuwa na kikomo au kazi maalum. Lazima mkataba wa ajira uwe umeandikwa ukiwa unampa mfanyakazi huyo kufanya kazi nje ya Muungano wa Jamhuri ya Tanzania.
Mkataba wa ajira lazima ueleze maelezo yafuatayo. Jina, umri, anwani ya kudumu na jinsia ya mfanyakazi; mahali pa kuajiriwa; ufafanuzi wa kazi; tarehe ya kuanza; aina na muda wa mkataba; mahali pa kazi; saa za kufanya kazi; ujira, mbinu ya hesabu yake, na maelezo ya faida aiu malipo ya aina yoyote, na suala lingine lililofafanuliwa. Hata hivyo, ikiwa vipengele hivi vimetolewa tayari katika mkataba wa ajira, huenda mwajiri asijaze hali iliyoandikwa ya vipengele vya ajira.
Lazima mwajiri ahakikishe kwamba vipengele vyote vilivyoandikwa vimefafanuliwa wazi kwa mfanyakazi kwa njia inayoeleweka na mfanyakazi. Ikiwa kuna mabadiliko yoyote katika kipengele chochote kilichoandikwa, mwajiri anahitajika kupitia upya vipengele vilivyoandikwa kwa kushauriana na mfanyakazi ili kuangazia mabadiliko hayo. Lazima mwajiri amfahamishe mfanyakazi kuhusu mabadiliko hayo kwa kuandika.
Mwajiri anawajibika kuweka vipengele vilivyoandikwa kwa kipindi cha miaka mitano baada ya ajira kuisha. Ikiwa mwajiri atashindwa kutoa mkataba ulioandikwa katika kesi zozote za kisheria, mzigo wa kuthibitisha au kukataa masharti fulani ya ajira uko kwa mwajiri. Kila mwajiri lazima aonyeshe taarifa ya haki ya wafanyakazi katika mahali panapoonekana.
Chanzo: Sehemu ya 14-16 ya Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ya 2004.
Mkataba wa kazi wa kipindi maalumu
Kwa mujibu wa sheria za kazi za Tanzania, ni marufuku kuajiri mfanyakazi kwa kipindi cha muda maalumu uliotajwa kwa kazi zenye asili ya kudumu. Mkataba na mfanyakazi utakuwa wa aina kati ya zifuatazo-(a) mkataba kwa kipindi cha muda usiotajwa; mkataba kwa kipindi cha muda kilichotajwa kwa kazi za wataalamu na mameneja, mkataba wa kazi maalumu. Hakuna sehemu yeyote kwa mujibu wa Sheria ya ajira na mahusiano kazini ya 2004 inayotoa maelezo juu ya kuendeleza mkataba au muda wa juu wa mkataba wa kipindi maalumu.
Ikiwa mfanyakazi ataendelea kufanyakazi baada ya kipindi maalum kuisha, haki na majukumu hubaki sawa, bila kuwa kwa makubaliano yoyote yanayopinga, kama yalivyokuwa mwisho wa kipindi. Ikiwa hakuna muda maalum wa ushirikiano, mwezi yeyote anaweza kubainisha ushirkiano wakati wwote baada ya kutoa ilani ya lengo lake kwa wenza wale wengine.
Chanzo: Sehemu ya 14 ya Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ya 2004. Sehemu ya 197 na 200 ya Sheria za Mkataba Kifungu cha 345
Kipindi cha majaribio kazini
Sheria za kazi katika Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ya 2004 hazisemi wazi ni kwa muda gani mfanyakazi atakuwa katika majaribio kazini chini ya mwajiri wake. Hata hivyo, sheria hii inatamka japo si wazi sana kwamba Mafanyakazi mwenye chini ya miezi 6 kazini iwapo ataachishwa kazi hawezi kulalamika kuwa ameachishwa kwa hila.
Chanzo: Sehemu ya 35 ya Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ya 2004
Taratibu/mwongozo wa hali za ajira
  • Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini Sehemu ya 6 ya 2004 / Employment and Labour Relations Act, No. 6 of 2004
  • Sheria ya sikukuu za kitaifa, 1966 / Public Holidays Ordinance, 1966
Kuhusiana mada

Sunday, 20 November 2016

matangazo ya msp




]
MASATU SERVICE PROVIDER
S.L.P ……...  BUNDA
0684112154/0752678604
INAPENDA KUWATANGAZIA HUDUMA MBALIMBALI TUNAZOTOA KAMA IFUATAVYO:-
MASATU SERVICE PROVIDER
Ø KUCHAPISHA MAPACHISHO YOTE
Ø KUTENGENEZA KADI ZA HARUSI,VIKUNDI ,MWALIKO,MICHANGO & DESIGNING
Ø KUTENGENEZA VYETI VYA MATUKIO MBALIMBALI ( CERTIFICATE DESIGNING)
Ø KUPIGA PICHA AINA YA ZOTE ( PASSPORT SIZE EXPRESS) NA KUSAFISHA
Ø HUDUMA ZA KURUDUFU AU KUANDIKA MAANDISHI AINA ZOTE ( HUDUMA YA PHOTOCOPY & PRINTING)
Ø SCANNING
Ø TUNACHOMA NYIMBO KWENYE CDR / DVDR, MEMORY CARD & FLASH
Ø TUNAUZA HOUSING ZA SIMU,BETRI ZA  SIMU, FLASH, CDR / DVDR, MEMORY CARD & KADIRIDER ZA MEMORY
Ø HUDUMA YA ODERING YA KIFAA/KITU CHOCHOTE


KARIBUNI SANA TUPO CHITARE CENTER

Saturday, 19 November 2016

MAWASILIANO


KWA LOLOTE USISITE KUWASILIANA NASI

Email:masatusobago23@gmail.com
Tell:0752678604
0684112154
0627619981
0676175594